Je wewe  ni mtu mwenye furaha? Au hofu na hatia huondoa  furaha yako yote? Je,ungetamani kuondoa hatia yako, lakini  kwa njia gani? Huenda unajiuliza , je, nitakuwa mwenye furaha tena?.
 Ninayo habari   njema kwa ajili yako. Kuna mtu mmoja awezae kukusudia , kusamehe dhambi zako , na kukupa furaha  ya daima. Jina lake ni Yesu. Ngoja nikuambie habari zake.
Mungu ndiye huyo mmoja aliyeumba ulimwengu . Vyote aliviumba ulimwenguni. Alikuumba wewe na mimi.
Mungu akupenda . yeye humpenda kila mmoja ulimwengu. Mungu atupenda sabna hata alimtuma Yesu mwanae pekee ulimwenguni. Yesu alipokuwa hapa Duniani aliponya wagonjwa; aliwafariji wenye huzuni. Alifungua macho vipofu . Aliwafundisha watu mambo mengi. Tusome  habari katika Biblia.
Yesu alitutaka tuelewe upendo mkubwa alio nao Baba yake kwa ajili yako na mimi. Alisema hadithi hii iliyoelezea upendo huo nao Baba yake.  Mtu mmoja aliishi mjini kwa furaha na wana wake wawili alidhani yote ni salama . Siku moja , mmoja wa wana wake aliasi na kumwambia, spendi mji huu, nataka kufuata njia yangu mwenyewe na kuondoka. Nigawie urithi wangu.  Baba aliuzunika sana , lakini alimpa fedha  na kumruhusu aende . Alijiuliza, je, nitamwona mwanangu tena? Kwa nini mwana alikuwa muasi hivyo?
Mwana alienda mbali na kujifurahisha kwa hela yake na rafiki zake. Alifuja fedha zake na kufanya mabaya mengi. Alidhani amepata wakati mzuri hata kwa ghafla fedha zake ziliisha na rafiki zake walimwacha. Kisha walimwaacha yeye pekee na ailjiona mwenye hatia sana  je, angefanya nini?
Alimwendea mkulima alimpeleka kuchunga nguruwe. Hakupewa chakula cha kutosha. Alikuwa na njaa sana hivyo alitamani kula chakula cha nguruwe . Alianza kufikilia maovu yote aliyofanya na jinsi alivyomtendea Baba yake.  Alizidi kupata uchungu zaidi.
Siku moja ,alikumbuka Baba yake jinsi alivyokuwa mwenye upendo na jisi alivyopendwa alipokuwa nyumbani. Alifikiri je, ningerudi  kwa Baba yangu baada ya kumtendea haya yote? Je, bado angenipenda ? sistaili kuwa mwana  wake. Ikiwa angenipokea ningekuwa tu kama mjakazi wake nyumbani kwake.
Kwa ghafla alisismama na kuanza safari ya kurudi nyumbani kwa Baba yake . Angeona kama Baba yake bado angempenda .  Baba alitamani mwana wake tangu alipotoka. Alijiuliza , je, mwana wangu atarudi tena?
Baadaye siku moja alimwona mtu yuko mbali anakuja. je, anaweza kuwa mwanangu? Alimkimbilia na kumkaribisha nyumbani kwa mikono ya ukarimu. Alisema , mwanangu huyu alipotea lakini sasa amepatikana. Sisi sote tumekuwa kama huyu mwana , sote tumetoka kwa Baba yetu mbinguni. Tumeharibu muda na mema yote ambayo ametupa . Tumefanya maovu na kumwasi leo,  Baba yetu wa Mbinguni anatutaka tumrudie .
Anatungojea kwa mikono ya ukarimu . Je, tunaelewa upendo alio nao Yesu kwa ajili yetu? Baada ya kufundisha hapa Duniani  kwa miaka mitatu , aliwaacha watu waovu kumpingilia misumari msalabani. Aliona maumivu na kuachwa alipokuwa anakufa na kumwaga Damu yake kama Sadaka kwa ajili ya dhambi za Dunia yote.
Tunapokwenda kwa Baba , tunamwomba atusamehe Dhambi yetu. Atuonapo tumehuzunikia Dhambi zetu kwa Damu yake aliyomwaga .  Jinsi gani njia hii ilivyo ya ajabu. Yesu amekuwa Mwokozi wetu. Tumezaliwa upya na kuwa mtu mpya. Uzima unayo njia mpya . Yesu amebadilisha hatia  na hofu yetu kwa furaha na shangwe.

 MWOKOZI KWA AJILI YAKO


Share To:
Magpress

Calvin Petro

Kwa Moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na Maagizo yako. Moyoni mwangu nimeliweka Neno lako Nisije nikakutenda dhambi. (Zaburi 119:10-11).

Post A Comment:

0 comments so far,add yours