Hakuna jambo linaumiza kama kusalitiwa na mtu uliyempenda na ukamuamini mfano mzazi, mke, mume, mchumba, mtoto, kaka, dada au rafiki wa karibu. Maumivu yake huwa ni makali sana na huweza chukua muda mrefu sana kupona.

ZAB. 55:6-7, 12-13
“Nikasema, Ningekuwa na mbawa kama njiwa, Ningerukia mbali na kustarehe.  Ningekwenda zangu mbali, Ningetua jangwani.  Kwa maana aliyetukana si adui; Kama ndivyo, ningevumilia. Aliyejitukuza juu yangu siye anichukiaye; Kama ndivyo, ningejificha asinione.    Bali ni wewe, mtu mwenzangu, Rafiki yangu, niliyejuana nawe sana.”

Unaweza jaribiwa kurudisha kisasi au kumchukia huyo mtu kabisa. Lakini biblia inatukumbusha kuwa Yesu naye alijaribiwa kama sisi lakini hakutenda dhambi.

EBR. 4:15
“Kwa kuwa hamna kuhani mkuu asiyeweza kuchukuana nasi katika mambo yetu ya udhaifu; bali yeye alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote, bila kufanya dhambi.”


Hivyo unapokuwa umesalitiwa na ndugu, mwendee Yesu yeye awezaye kuponya mioyo iliyojeruhiwa na kukupa moyo wa msamaha na kuachilia. Yesu alisalitiwa na mtu wake wa karibu, anajua maumivu ya usaliti na pekee ndiye awezaye kukuondolea maumivu hayo na kuuponya moyo wako. Usijaribu kutafuta suluhisho mwenyewe maana hutalipata, mkabidhi Yesu, lia mbele zake na hapo furaha yake itakuwa nguvu yako.




Share To:
Magpress

Calvin Petro

Kwa Moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na Maagizo yako. Moyoni mwangu nimeliweka Neno lako Nisije nikakutenda dhambi. (Zaburi 119:10-11).

Post A Comment:

0 comments so far,add yours