Kutunza ujana, ndoa, uzee au wokovu wako ni wajibu wa mtu mwenyewe.  Ni kweli Mungu anatutunza na anayosememu kubwa katika kila rika la maisha yetu; lakini amempa mwanadamu ufahamu na utashi na anao wajibu wa kufanya ili kujitunza. 

Ili kuutunza ujana wako ni lazima ujue na uyazingatie mambo muhimu yafuatayo:
1.     NIZIJUE CHANGAMOTO ZINAZO KABILI KIJANA.
i)      Kwenda na Wakati–Biblia inaagiza kuukomboa wakati-Waefeso 5:15-16    Ni changamoto kwetu na ni fursa kutumia nguvu ya msalama kuishinda hii     
kawaida ya Dunia hususani vijana kuvutwa katika kwenda na wakati.  Kijana huvutwa na kushawishika kwenda sawa na wakati katika maeneo mengi.  Kijana anavutwa na kuvaa, kusuka, kunyoa, kutembea, kusema, kutenda sawa na wakati, hata kumiliki vitu vinavyoendana na kuendana na wakati. Dunia inavyotuvuta katika kwenda na wakati, Biblia inatuagiza kuukomboa wakati.  Kuukomboa wakati ni kutumia vizuri wakati tuliopewa kama fursa ya pekee.  Wakati wa Ujana ni wa kuwekeza vitu vya rohoni na mwili, komboa wakati.
a)    Komboa wakati Ki-Elimu: Usipoteze wakati kwa mambo yasiyokuhusu, mfano kijana mwanafunzi Soma kwa bidii ni wakati wake, siku ikiisha jiulize umeongeza nini ki-elimu? Usiishi kiholeholela tu fursa hiyo inapita.

b)    Komboa wakati Ki-Uchumi: Usipoteze wakati kwa matumizi ya kipuuzi, fasheni za mavazi, mitindo ya nywele, hata kijiko huna, wewe unavaa tu. Komboa wakati ukijua kuna kuoa na kuolewa lazima ujipange mapema. Siku ikiisha, wiki, mwezi, mwaka Jiulize umeongeza nini kiuchumi? Kumbuka kuna miaka saba ya shibe na miaka saba ya njaa lazima uishi kwa adabu/hekima, siku zijazo huna nguvu ya kuwekeza kama UJANANI.

c)     Komboa wakati Kiroho: Usipoteze wakati Kiroho, tumia fursa hii vizuri. Siku inapoisha, wiki, mwezi, mwaka, kijana jiulize umeongeza nini Kiroho.  Umeongeza nini ufahamu katika Neno la Mungu, Umeongeza nini Maombi, Umeongeza nini utumishi wako wakati huu una nguvu, usiishi kiholela. Wekeza vitu vya Ki-Mungu ndani yako, funga na kuomba, soma neno, tumika kadri uwezavyo. Ukifika uhitaji yamkini hata huwezi kuomba sana unaakiba ya kutosha ya Maombi/Neno la kusimamia kupita kipindi hicho.

d)    Komboa wakati-tumia vizuri fursa ya kuwa kijana - 1Nyakat 12:32 Kwa kufanya mambo yakupasayo kufanya wakati huu (ujanani) kila eneo. Wakati ujao ukifika hata ukitaka kurudidarasani akili haitunzi tena kumbukumbu kama leo na majukum yataongezeka, ukitaka kubeba zege huwezi huna nguvu kama leo, Kiroho vivyo hivyo, ukisoma Neno ufahamu unachoka haraka, kufunga huwezi tena. Uwe na akili zijue nyakati.

ii)    Tamaa za Ujanani – 2Tim 2:22, Mith 27:2, 1Kor 6:18a, Wimbo 3:5
Ni changamoto kwetu na ni fursa kuonesha nguvu ya msalaba kutiisha mwili.
Kijana anavutwa sana na tamaa za ujanani na hizi zinamkumba kijana si kwa sababu hayuko kiroho hapana, zinamkumba kwa vile ni kijana.  Changamoto hii tunaipata wote, vijana waliookoka na wasiookoka ila tofauti yetu ni katika kuzi-hundle Kijana aliyeokoka anazitiisha na asiyeokoka anazitii tamaa hizi.

Biblia imetaja moja kwa moja kuwa ni tamaa za ujanani na zinawakumba vijana wote na lazima kuzitiisha zisubiri wakati [NDOA].

NI MUHIMU KUYAJUA, KUYAELEWA NA KUZINGATIA MAMBO 4 YAFUATAYO: -
a)     Uhai wa milango ya fahamu kwa kijana ni tofauti na rika nyinginezo.
Milango ya fahamu ni Macho, Maskio, Pua, Mdomo, Ngozi-inauhai [active]. 

b)    Uhai wa hisia za mwili kwa kijana ni tofauti na rika nyingine. Unatokana na mabadiliko ya mwili yaliwekwa na Mungu mwenyewe.

c)     Upo Uhusiano wa karibu kati ya Hisia za mwili wa kijana na Tamaa za ujanani, hili lazima kijana alijue ili ajilinde.

d)    a, b, na c hapo juu, zinatusaidia kujua sababu ya Mungu kutuagiza watu Kukimbia tamaa za Ujanani, tusichochee mapenzi mpaka Ndoa.

iii)  Inaagiza kwa msisitizo kusema zikimbieni tamaa za ujanani/mwili.  Tumeongea na vijana wengi walioanguka hawakupanga kuzini. Ila wamezembea katika kulitii Neno la Mungu badala ya kukimbia wao wanakaa, wanaleta hoja, wanakemea, wanaomba, wanapinga mwisho wa siku wanajikuta chini, kwa ukaidi wao kwa Neno la Mungu. Biblia haikushindwa kusema kemea, ombea, pinga ila imesema KIMBIA.

iv)  Usichochee mapenzi, usizichochee hisia za mwili/matakwa ya mwili.          
v)  Milango ya fahamu ikichochewa inazalishahisia katika mwili;
vi)  Hisia/Msisimko wa Mwili wa kijana ukichochewa unazalisha uhitaji;
vii)  Uhitaji wa Kimapenzi ukichochewa unazalishaTamaa za Mwili;
j)  Tamaa za Mwili/Ujanani zenye msukumo mkali kutaka kukidhi uhitaji zikichochewa zinalet anguko, mauti; Kijana hatua hii hakumbuki wokovu, huduma, aibu, magonjwa yanayotokana na zinaa-Kaswende, kisonono wala Ukimwi. Hakumbuki mimba au watoto wasiotarajiwa. Anahaha kutaka kukidhi uhitaji wa mfalme/malkia wake tu, ni hatari.
k)  Mauti inazaliwa kutokana na Tamaa iliyopembejewa na Kijana. Kuna Kijana alizilea hatua tulizojifunza hapo juu, hakuchukua hatua za Kiroho kuutiisha mwili akajikuta anabaka-wadada na wakaka wote wanabaka japo hapo tunamuona kaka amebaka – 2SAMWELI 13:1-22. Biblia inasema wazi unaingamiza nafsi yako mwenyewe-Mithali 6:32.

Kuyalea na Kuyachekea mambo hayo juu ndipo unaskia anguko, Kijana anayeheshimiwa na Mungu na watu anajikuta amezini. Unapokosa subra na kuparamia unalala na mke au mume wa mtu kiuumbaji. Kimsingi kila mtu ameumbiwa mume au mke wake – Mwanzo 2:22.

iii) Vichocheo vya mapenzi/tamaa za ujanani/tamaa za mwili
Ni changamoto ya tatu inayotukabili vijana na lazima tuishinde ili tusalimike. Ni muhimu kujua vichocheo vya mapenzi/tamaa za mwili ili kuviepuka.  Nisipojuavichocheo hivi si kiroho bali ni ujinga unaotishia usalama wangu.

Vichocheo vifuatavyo huyaamsha mapenzi, huchochea tamaa za mwili: -

a)    Kuzitafakari/kusikilizia hisia za mwili-Inahusisha ufahamu wenyewe
Biblia imetuagiza tuyatafakari yaliyo juu-Wafilip 4:8. Mungu alijua tukiyatafakari ya chini yakiwemo tamaa za mwili tutachochea mapenzi.

i)  Usijiulize maswali ya kipuuzi mf. ‘Hivi, tafika kuoa au kuolewa bila kuonja? Wenzio walioonja wamekuwa watumwa wa dhambi hiyo kujitoa ni gharama kubwa wengi wameshindwa kuilipa, usiwaze kuonja hadi NDOA.

ii)  Baridi imezidi/Upweke jamani niko peke yangu. Ulitaka uwe na nani? Haya ni majira ya Bwana yenye kusudi timilifu uwe peke yako, wakati wa kuwa 2 na 12 watakapokuja hao wa kike na wa kiume-utakuja tu, vumilia.

b)    Kusoma makala za mapenzi [makala za Internet, magazeti, vipeperushi, vitabu]-inahusisha macho yanayosoma makala.
·        Unashangaa binti au kaka anasoma vitabu vya tendo la ndoa/Mapenzi.
·        Internet Café anaenda kutazama mambo ya Ngono/Mapenzi. n.k.
Kijana huyu atakuwa salama kweli au ndio hao mwisho anabaka mtu.

c)     Kutazama mambo ya ngono au yanayohusu ngono-inahusisha macho.
Mikanda ya x, sinema za x, picha za x hasa kwa internet na hata ‘live’ kuna watu wanapenda kuchungulia sehemu zenye upenyo wa kufanya hivyo.  Raha yake aone tu utupu wa watu na mchezo unavyokwenda, atapona?

d)    Kushika au kushikana/kugusana-inahusisha ngozi-Wakolosai 2:21.
·        Mkono unaganda dk.5 dada na kaka wanasalimiana salamu yetu.
Mkono wako una chapa ya Yesu usiruhusu kujinajisi kwa kutii mwili.
·        Vidole vinaongea kwa kupapasa au kubonyeza au kutekenya ni uchochezi.
Vidole vyako vinachapa ya Yesu, usiruhusu kujinajisi kwa mambo hayo.
·        Tongue Kiss/Denda ni hatari wala mtu asijifariji kuwa salama-usionje.
Ulimi wako unachapa ya Yesu usionje uchafu [mate] subiri Ndoa utanyonya mpaka uchoke ukitaka maana utakuwa huru katika hayo si leo.
·        Ngozi ikiskia umeshika/kwa, unapapasa/swa, umekula denda, lazima itashtuka na kuleta hisia ya kuvutwa katika ngono kwavile wewe ni kijana. Usiidhalilishe Chapa ya damu ya Yesu uliogongwa siku ulipookoka, itunze.

e)     Kusikiliza mambo/maneno ya ngono au yanayohusu ngono-sikio.
Sikio lako linachapa ya Yesu usilisikizishe uchafu wowote-ni kichocheo.
Kusikia ni sikio kupata jambo bila kukusudia lakin kusikiliza ni kukusudia. Hata kama sikio limenasa uchafu kwa bahati mbaya hakikisha unalitoa.

f)      Kuongea mambo ya ngono au yanayohusu ngono-inahusisha mdomo.
·        Mazungumzo ya Mdomo ni hatari-Mithali 6:26; 7:16-18,21. Iko nguvu katika midomo/maneno. Biblia inasema Maneno huzaa uhitaji na sura hiyo hiyo ya 6, inashauri jiepushe na midomo ya malaya; Kwa maneno alimshinda-si kwa mtutu, si kwa ‘hug’ wala busu ni maneno tu na akamshinda. Usiruhusu kupokea maneno hata ya mzaha kuhusu ngono.
·        Mawasiliano katika Simu ni vema kuangalia sana unavyoenenda.
Idadi ya “Call au Sms” mfano kutwa mara tatu unampokea Fulani.
Simu inazidi ‘dose’ ya Panadol kutwa mara tatu yeye mara tano.!!
Muda wa “Call au Sms” mfano usiku sana au alfajiri ni kichocheo.

Usiruhusu Simu za usiku wa manane/alfajiri hata kwa manadai ya kuamsha ktk maombi kwa muda huo ataamsha na vingine si maombi tena!
Sauti ya “Call” kuna sauti za uchochezi mfano kulegeza, kuguna, kutetemesha sauti, sauti kama analia na nyinginezo kwa kijana utajua tu.

·        Mazungumzo “Simu au Sms” yakihusu ngono ni uchochezi sana.
Mambo hayo juu hata kama mtu hajaweka neno la kimapenzi/kimahaba ni kichocheo, Je, mazungumzo yenyewe hayo ni hatari zaidi mara 100.

Biblia inaonya mazungumzo mabaya yanaharibu tabia njema-1Kor 15:33.
Mfano: Naskia baridi njoo basi unipe joto, wewe umekuwa ‘heater’?
Najiona mpweke ‘lonelyness’ afadhali uje hapa nichangamke. Kweli wewe una Baba, Mwana na Roho Mtakatifu bado mpweke?
Ukiyachekea hayo, hutaki kuyakemea, anaongeza ‘dose’ sasa utaambiwa wazi zaidi ‘nina nyege, ni wewe wa kutoa nyege zangu’

g)    Zawadi ni moja kati ya vichocheo vya mapenzi kwa namna hii.
·        Size ya zawadi    -   Ukubwa, zawadi ya thamani kubwa. Itaua msimamo.
·        Idadi ya zawadi  -   Wingi vitu tele unapokea au mara nyingi-utalipa tu.
·        Aina ya zawadi   -   Kitu gani unapokea-chupi? Zawadi hiyo itaongea tu.
Msimamo wa Semina hii ni USITOE NA USIPOKEE ZAWADI. Tunaishi zama za uovu, usanii na malaghai mpaka Kanisani wa kike/kiume wao wanajua kuipaka asali nia yao ili usishtuke mapema mpaka umefika chini, zawadi ni chambo kukunasa we.  Hutaki Kanuni hii yatakayo kupata usilie.
Wachumba: Vijana hawa wako huru kutoa/kupokea zawadi ila Kanuni ni hizo hizo hapo juu. Uchumba si Ndoa muda huo bado unaendelea kumthibitisha Mungu, usijeishia njianiukalilia mtu na vitu vyako.

h)    Picha na Mikao ya Picha kwa jinsia mbili ni Kichocheo cha Mapenzi.
·        Picha za nusu uchi eg. Kifua/Tumbo/Mapaja wazi au chupi/sidiri tu.
·        Picha za utupu [mwili wote], picha hii hana nguo hata moja-ni kichocheo.
·        Picha na Mikao yake inavunja miiko ya jinsi ya kuenenda Vijana waaminio.
‘Pouse’ la Kushikana Mabegani, Kushikana Viuno, Kushikana Kifua mtu anajikuta ameshika matiti katika pouse la picha, Kushikana Makalio, Kubusiana Shavu au Mdomo, Kupakatana/Kukumbatiana ni KICHOCHEO. Kijana usikubali Kuidhalilisha Chapa ya Yesu kwa Pouse la Picha.

i)      Mavazi ya Vijana wa Kike na Kiume yanavyokuwa Kichocheo.
·        Mavazi ya Kuonesha Nguo za Ndani-Milegezo, Vifungo wazi, Mipasuo n.k.
·        Mavazi ya Kuonesha Maungo/Maumbile-Kubana sana inachora umbile, Kuangaza [transparent] inaonesha viungo vyote japo kavaa, ni vichocheo.
·        Mavazi ya Kutositiri Mwili-Nguo fupi-pensi/bukta/skert/gauni/blaus, Nguo hizi huacha Kifua wazi, matiti nje, Kitovu nje, Tumbo nje, Kiuno nje, Kwapa nje-ndio unakuta kijana haabudu anachungulia titi kupitia kwapa.

·        Ni maombi yetu mavazi hayo yasivaliwe nawe unayesoma makala hii. Ni maombi yetu uushinde mwili, endapo utakutana na mavazi hayo kazini, shuleni, kwenye daladala, barabarani, dukani, sokoni na hata Kanisani kwa Waongofu Wapya au Wakongwe wenye mitazamo tofauti. Utaona hatuwezi kuepuka hili moja kwa moja kwa jamii yetu ila tumejifunza ili ukiona mavazi hayousi-‘take advantage’, usikodolee macho mpaka mate yanatoka huna habari ni hatari kwa afya yako, epuka.

j)      Mazingira hatarishi/njia kuu ni Kichocheo - Mithali 7:7-13a, 21-23.
Njia Kuu ni mahali pa Kificho, Gizani, Uchochoroni, Chumbani, Ufukweni, Kuwepo wawili tu mnataka kufa maana mazingira tu ni kichocheo tosha.
Kabla ya kugusana, mabusu, zawadi, mazungumzo vyote hivyo bado, ile kuwa wawili tu maeneo hayo ni kichocheo tosha na kinaongea kwa kasi.

Kijana mmoja mjinga yeye alizubaazubaa NJIA KUU yaliyomkuta ni balaa.
Tunapomalizia kichocheo cha 10 cha mapenzi hebu tusome andiko hilo.
Kijana huyu alitembea muda hatarishi kwa kijana, akakaa mahali hatarishi, akakutana na mtu hatarishi [kahaba], akaambiwa maneno hatarishi, akanaswa. Mithali 6; inatoaushauri kuwa jiepushe na maneno ya Malaya n.k. ndipo sura ya 7; inaonesha kwa maneno ya ubembelezi tu kahaba akamshinda Kijana kiulaini kabisa akaongoza njia kama Ng’ombe aendavyo machinjioni uhitaji umeshapamba moto, mfalme amesimamisha majeshi hayarudi chini, anaona nikidhi tu uhitaji wa mfalme nisalimike, kumbe maskini anaiangamiza nafsi yake ya thamani-Marko 8:34-35.   

Tunaishi zama za uovu makahaba wa kike/kiume wapo Kanisani pia.  Makahaba hupenda NJIA KUU soma Ezekiel 16:22-26. Ni mahodari wa ubembelezi, kwa kiroho cha kusuasua cha kutozingatia mipaka ya uhuru wetu, hutoki, utalainika mwenyewe na utajikuta unaongoza njia kama kijana mjinga. Epuka mazingira hatarishi, kuna kisa kilitokea Kanisani mkesha wa Vijana wa Maombi ya masaa 48. Kaka kamfata dada anamwambia “nina nyege na wewe ndio wa kutoa nyege zangu” Ikiwa mkesha wa maombi kuna watu wanamawazo hayo, je, huko njia kuu?   

Umejua vichocheo 10, usichochee. Ukifanya uzembe umenaswa hatua No.1 Mlango wa fahamu umepokea taarifa-Itoe mapema, ikiwa uko hatua No.2 ya hisia/msisimko wa mwili pambana-usipembejee, kama ni hatua No.3 ya uhitaji usimridhie mfalme/malkia tiisha hali hiyo, usifikie hatua No.4 ya kuwaka tamaa ni mbaya sana inapelekea hatua No.5 ya MAUTI.

2.     NIJUE JINSI YA KUZIKABILI CHANGAMOTO KWA MUJIBU WA BIBLIA

Tumeona Changamoto 3 katika Somo hili, Kwenda na Wakati, Tamaa za Ujanani na Vichocheo. Hizi ni changamoto kali kwetu ukitumia akili utachemsha. Ufuatao ni muongozo kidogo tu wa kukabiliana na Changamoto hizo kwa mujibu wa Biblia:

i)      Maombi-Uwe na maisha ya maombi, ombea ujana wako siku zote-Luk 18:1;
 Tabia ng’ang’anizi Funga na Kuomba na utapata upako wa kuutiisha mwili.
ii)    Neno la Mungu likae kwa wingi ndani yako ili usafishe njia zako-Zab 119:9.
iii) Nikubali na niamue kwa dhati kuusulubisha mwili/kuunyima matakwa yake.
·        Utu wa kale ni wakati mwili ulipokuwa na nguvu, ukiokoka-Rum 6:6;12:1
Kama utu wa kale unakung’ang’ani jichunguze pengine hujauvua vizuri- funga na kuomba utoke-Math 17:21. Umvae Kristo-Rumi 13:13-14.

·        Kuishi kinyume na mwili na tamaa zake na mawazo yake-Galatia 5:24.
·        Paulo aliamua kutesa mwili, wewe na mimi je?  1Kor 9:27; Marko 8:34-35;
Ukitaka kuiponya nafsi ati mwili unahaha, mfalme amesimamisha majeshi au malkia anahaha acha niiponye nafsi yangu kwa kukidhi uhitaji huu, maskini unaingamiza nafsi yako wala huiponyi kama unavyodhani. Na ukiamua kuiangamiza nafsi yako kwa ajili ya Kristo UNAIPONYA. AMEN.

iv)  Nijitenge na ubaya wa kila namna yaani ubaya wote-1Thesalonike 5:22.
Tangu mwanzo wa somo hili tumeutaja ubaya mwingi tu na tumeujua EPUKA.
·        Kujiepusha na marafiki wabaya iwe waaminio/wasioamini-2Kor 6:14-18.
·        Kujiepusha na mazungumzo–Mith 18:7;1Tim 5:20;1Kor 15:33; Kol2:20-21.
·        Kujiepusha na Elimu na Hekima ya Ulimwengu huu ambayo ni upuuzi kwa Mungu-Efeso 4:13-14; Rumi 16:19 2Tim 2:11-22; 2Kor 10:5; Yakobo 3:17.
Elimu ya jumla ni nyingi moja wapo ni huwezi kuokoka duniani. Elimu ya Kristo inasema wazi watakatifu walipo Duniani ndio waliobora-Zab 16:3.
Elimu iliyotawala ulimwengu huu inayogusa vijana na baadhi wa Kanisani wameipokea na kuiamini, maana yake hawaamini nguvu ya msalaba ni: -
Huwezi kuishi KIJANA mwenye afya bila kufanya mapenzi kabla ya ndoa!!
Huwezi kuoa au kuolewa BIKRA kwa karne hii ‘Mary type’ hakuna leo!!!
Vijana wamepokea Elimu ya Kwanza ikazalisha Elimu ya Pili, ona juu. -Shetani anajua wakipokea tu Elimu hizi na kuziamini zitawakatilia mbali. -Watakata tamaa ya kujitunza kwamba sawa na bure, na wengi wamenasa. -Kumpata Bikra mwenzio huwezi, bora na wewe jichanganye; wamenasa.  -Kufika hadi Ndoa ukiwa BIKRA haiwezekan ananesha vichocheo, ananasa. Kwa nini ung’ang’ane na Elimu ya Dunia na kuamini na wewe si wa dunia?
Elimu ya Kristo iliyosema yasiyowezekana kwa wanadamu kwa Mungu yote yanawezekana mbona hiyo huiamini na kuitumia ili ukaishi.
Elimu ya Kristo iliyosema mwili si kwa zinaa pia siijui-1Kor 6:13.
Nikijawa na Neno la Mungu [Elimu ya Kristo] nitashinda-Zab 119:10.

v)    Nijue kuwa niliumbwa Kutenda Mema nisijifariji kuutii mwili/elimu-Efes 2:10
Kwa vile niliumbiwa utakatifu Biblia inanitarajia nijizuie -1Kor 9:25.
vi)  Mtazamo wa Mungu kwangu Kijana ni tofauti kabisa na ninavyodhani.
·        Rika ya ujana natarajiwa kumkumbuka/kumuabudu Mungu  Mhubiri 12:1.
·        Nizo nguvu si za ugali na maharage bali za kumshinda muovu-1Yoh 2:13-14.
·        Kwanini Mbingu zinaona kijana nina nguvu na nimemshinda muovu?
·        Ninauwezo wa Kufunga siku nyingi, kuomba kwa muda mrefu bila kuchoka,
·        Kusoma/kujifunza na kutafakari Neno la Mungu na kuliweka moyoni,
·        Kutumika kwa nguvu zangu zote hata sina muda wa kupoteza ila kukomboa. 
·        Nguvu za Kiroho zinapatikana katika hayo hapo juu, adui atakupataje?
Nguvu za Kiroho zinakusaidia kuushinda mwili, changamoto, dunia n.k.
Nguvu za Kiroho zinakuweka karibu na Mungu na adui lazima akukimbie
Nguvu za Kiroho zinakupa ufahamu wa kumjua Mungu na Neno lake.
Nguvu za Kiroho zinanipa uwezo wa kumuamini Mungu si wanadamu.
Nguvu katika Roho Mtakatifu na kuwa chini ya uongozi wa Mungu.

Nawaandikia ninyi vijana kwasababu mnazo nguvu, hata nguvu za kimwili tulizopewa pamoja na kutusaidia kiuchumi, elimu pia zipo kutusaidia kupata nguvu za Kiroho. Kijana usile mwaka mzima funga, omba kwa afya Kiroho/mwili.
Tangu siku za Yohana Mbatizaj Ufalme wa Mungu unapatikana…. Math 11:12.
Ili upate vitu vya Ufalme wa Mungu lazima uwe na Nguvu si kilegelege hivyo.
Ili kuteka kitu lazima umfunge mwenye nguvu, na ufalme ni hivyo kama mwili unanguvu utiishwe, hekima za dunia zitiishwe ili uteke vya ufalme-Math 12:29.
Ili uje upate mke/mume mwema aliyejaa nguvu hizo lazima uwe na nguvu.
Ili upate Baraka za Ki-Mungu hata kwa maisha ya kimwili lazima uwe na nguvu.
Kwahivyo, unahitaji nguvu ili kuutunza Ujana wako si kwa ulegelege. Nikizembea katika kutafuta nguvu nikajikuta nimezini yapo MADHARA yake.

3.ZIJUE BAADHI YA MADHARA [20] YA KUFANYA MAPENZI KABLA YA NDOA

i)      Kumtenda Mungu dhambi [Yusufu]–Mwanzo 39:6-9; Rumi 8:6-8; 1Kor 6:15-20.
ii)    Kuharibu ushuhuda [Wokovu unatukanwa] – [aibu] Mithali 6: 32 – 33.
iii) Kufungua Mlango wa mapepo/kupokea maroho ya unayezini nae – 1Kor 6:16.
iv)  Kuishi na Hatia Moyoni hasa dhambi isipotubiwa – [fedheha] Mithali 6:32-33.
v)    Kuishi na Majuto maishani maana kumbukumbu haifutiki – 1Kor 6:18 – 20. Dhambi hii inafanyika juu ya mwili wako ndio maana haifutiki. Toba ya Kweli Mungu atasamehe na kusahau-Ebrania 8:12, lakini wewe hutosahau kamwe.

vi)  Kujichukia na Kumchukia sana mtu uliyeanguka naye, misisimko yote itaisha-2Samweli 13:1-22. Kuna kisa cha kusikitisha cha Kijana Amnoni na Tamari.
vii)    Kuwa hatarini kuingia katika anguko tena-kwa mwili kudai haki yake kwa
Kasi maana umechokozwa.  Utaingiwa na roho ya kutoshiba-Ezekiel 16:28-30a.
viii) Kuua nguvu ya kujizuia, kuudhibiti na kuuweza mwili- 1Kor 6:13; 9:25. Ndipo mambo ya kuchua/kupiga punyeto [masterbation] yanapoingia Kanisani, malkia na wafalme bandia wanaponunuliwa na vijana kwa matumizi machafu. Kuchua, kutumia malkia/wafalme bandia ni ukahaba tosha-Ezekiel 16:15-17.

ix)  Kuwaumiza wazazi wako na Kanisa la Mungu wewe ni kiungo – 1Kor 12:12-26. Tunaudhaifu katika mapambano maana kiungo wewe umejeruhiwa na nafasi yako inaupungufu, pia tunaposimama kama Kanisa unatutia doa/dosari.
x)     Kutoaminika kwa Mungu, Wazazi, Kanisa na Kutojiamini-Maombolezo 1:8a.
xi)  Kupata Mimba/Watoto wasiotarajiwa; wote kaka/dada mnapata mimba/watot.  Ni aibu sana ukiwa Kanisani kupata/kutia mimba/watoto wasiotarajiwa.

xii)    Kupata magonjwa ya Zinaa Kaswende, Kisonono, Gonoria, Ukimwi n.k.
  Ni aibu kijana wa Kanisani kupata magonjwa ya zinaa akiwa Kanisani.
xiii)  Kuua ndoto zako. Ukishapata mimba/mtoto/ukimwi ndoto zinaishia hapo.
  Ndoto ya wengi ni kuoa au kuolewa akiwa bikra, asilale na mtu kabla ya ndoa.
Utaiua ndoto hii nzuri ya Ki-Mungu inayotaka kila mtu awe na mke/mume wake mwenyewe 1Wakor 7:2; Ilikusudiwa hivyo tangu awali-Efeso 2:10.

xiv)  Kulipa gharama kubwa ya kurudi katika nafasi yako kiroho na kimwili pia.
Kihuduma kurudisha viwango ni gharama kubwa, masomo kuanza tena ni gharama kubwa, kwa wazazi/jamii kukupokea kama mwanzo ni ngumu. Na BIKRA hiyo ndio utalipa gharama ya kukubali matokeo maana hairudi si kwa kijana wa kiume au wa kike uki-unsealed hakuna muujiza wa ‘resealed’.

xv) Kuchakaza maumbile yako wavulana/wasichana–Wimbo Bora 8:8,9,10.
Malkia-uke unaukuta[bikra] kwa kulala na mvulana tu ukuta unaondoka-8:8.
Ukuta ukitunzwa hadi ndoa ni heshima na furaha kwa Wazazi na Kanisa-8:9.
Ukuta ukitunzwa hadi ndoa ni heshima na kibali cha ziada kwa ‘mr’ wako-8:10.
Inatisha sana ukuta kuondoshwa binti akiwa ameokoka na yupo Kanisani.  Dada ambaye umeokoka huna UKUTA utunze UKUTA wa Roho Mtakatifu sasa. Na endapo utaolewa ukiwa umejitunza kwa jinsi hii kwa maumbile ya uke ‘mr’ wako atajua umejitunza hata kama UKUTA haupo.  Miaka yako katika WOKOVU ifanane na hali halisi ya Malkia wako. Sio Miaka 5 ya Wokovu lakini Malkia anaonesha ni Muongofu Mpya wamiezi 5 tu ya baada ya kuchumbiwa-AIBU!

Mfalme-uume unaharibiwa na wanawake/kupata jeraha-Mith 31:3; 6:32-33.

Kibinaadamu wakaka wanadhani wako salama kwa vile hawana alama ya wazi. Ki-Mungu Biblia inaonesha wazi kuwa wafalme wanaharibiwa na wanawake na kuna jeraha lisilofutika na kuvunjiwa heshima kwa kaka aliyezini. Kaka anatoka akili kila anavyozini na alama Mungu aliyoiweka kwa mfalme used haifutiki.   Mungu anatutaka wote wakaka na wadada tuwe BIKRA na INAWEZEKANA. Maswali ya wewe mzima yaulizwe kote kote si kwa dada tu. Biblia imetoa ‘Gender Balance’ juu ya hili na kuonesha madhara na matokeo ya kaka kuzini >Kutoka akili – aziniye na mwanamke hana akili kabisa, anaingamiza nafsi. >Jeraha na fedheha haitofutika – Mithali 6:32-33; 20 – 26; 7:1-15; 21-23. >Haifutiki moyoni maana hufanyika juu ya mwili wako wote – 1 Kor 6:18 – 20.  >Ni kweli kuwa kwa toba ya kweli Mungu atasamehe/atasahau-Ebrania 8:12. >Wewe hutosahau kamwe tendo hilo hata kama ni dk 5 tu, maana linahusisha >>Moyo wako wote, Akili zako zote, Nguvu zako zote na Mwili wako wote.  Na Inasikitisha kijana kuanza ngono akiwa tayari ameokoka na yupo Kanisani.


Nakupa pole unayejifariji kufanya dhambi hii ukidhani hawapo tena MABIKRA. Dhana hiyo haikuanza leo tangu waandishi wa makala hii tukiwa ‘single’ dhana ilivuma hawapo mabikra kumbe tupo na tukaoana tukiwa BIKRA kaka na dada. Na tumekutana na wanandoa wengi waliooana wakiwa BIKRA kaka na dada. Mabikra hawatakoma katika nchi maana katika kila jambo la Ki-Mungu masalia wataendelea kuwepo hata uovu uzidi sana. Kaka kuwa wa Kwanza kwa DADA na Dada kuwa wa Kwanza kwa kaka SIKU YA NDOA ni Jambo la Ki-Mungu. Ni Muhimu kuishi maisha ya uaminifu kamwe usijifariji kwa dhana hiyo potofu.

Ni wote tunapaswa kujilinda na kujitunza hadi NDOA – Mithali 5:1-5; 9:13-16. Sio Malkia watunzwe, Wafalme waharibiwe hakuna fundisho hilo katika Biblia. Dhambi ni dhambi kwa wote, misisimko ya mwili ni wote, uzembe wa kuutii mwili badala ya kuutiisha mnafanya wote, kwanini BIKRA awe dada tu?  Tunatamani tunapomaliza kipengele hiki cha kuchakaza maumbile ufunguke. Usiulize maswali ya upuuzi kwa mchumba wako, “Vipi dada wewe ni mzima” nawewe je, kaka ni mzima? Au unataka kuvuna usipopanda? Hakuna Kanuni hiyo kwenye Biblia-Wagalatia 6:7; Wakolosai 3:25. Umeondosha kuta za wasichana tele tena mpaka upo Kanisani, inafika kuoa unataka mzima atoke wapi? Kuna wenzio kuliko wewe ulipoondosha kuta 5 wao wameondosha 15.  Ukipata mchumba/mke mzima ni neema tu usiifanye ni Kanuni ya kusimamia.  Ikiwa umeomba na umempenda kwa dhati maswali yanatoka wapi? Upendo hustiri wingi dhambi 1Pet 4:8, Upendo una adabu-1Kor 13:5. Upendo wako vipi?

Mkazo huu ukuguse moyoni kaka/dada bikra muendelee kujitunza, uthamani wa Ubikra wako ni mtaji mkubwa kwa hatima yako ni zaidi ya fedha/dhahabu. Mungu amekuokoa, amekuwahiUSIICHEZEE NEEMA HIYO wengi wanaililia, jiombee sana huku ukizingatia yale mambo ya mwanzo wa somo ili kujilinda.

xvi) Kaka kupoteza mbegu za uzazi-unatoa wakati sio, kwa mtu siye, mahali sio.
       Dada naye anapokea mbegu za uzazi-wakati sio, kwa mtu siye, mahali sio.
       Wakati muafaka ni Ndoa, mtu sahihi ni Mwenzi wako, uchochoro huo sio.

xvii) Kaka/Dada wote kupoteza nguvu kwa kutumia kwa ngono hiyo-Mith 31:31
       Nguvu ambayo ingetumika kwenda kushuhudia inatumika katika ngono.

xviii) Dhambi hii ikilelewa na kijana mwisho hupelekea kutamani wake/waume
za watu. Kawaida ya uovu unakua, hukuweza kumuogopa Mungu na ukafanya ngono na wanafunzi wenzio Sekondari au vijana wenzio wadogo Kanisani mwisho unaona wake/waume za watu wote sawa tu na hao.  Kijana unaanza kumendea wake/waume za watu kwa kutotunza ujana wak.

Biblia imeonya vikali hapa, usidhani uko salama ni hatari-Mith 6:27-29. Inaonesha kuwa makali ya moto yatakuwa kifuani mwako, hauko salama. Wengin sawa na baba/mama yako unapata laana kuona utupu-Walawi 18:7
Vijana wengine huona ni bahati kuwa na mke/mume wa mtu hiyo ni balaa, nuksi, mkosi huo, kwanini uone sawa ku-share na mtu? Walawi 18:16;20.

xix)   Madhara ya Dhambi hii kwa Kijana hata akiingia katika Ndoa ni:
·        Dada atapata aibu kwani mumewe atajua kuwa hukutulia Kanisani alitulia siku chache karibu na kuolewa na pengine akawa na mimba isiyo ya ‘mr’.
·        Dada kutoaminiwa na mumewe na kuishi kwa mashaka katika Ndoa.
·        Kaka naye ikibainika hakutulia Kanisani mkewe hatomuamini ni hatari.
·        Mume/Mke kuua nguvu ya mguso wa upendo wa mvuto kwa T. Ndoa.
·        Kwa kuwa amezoea ku-sex na malkia/wafalme wengine Kanisani/nje.

xx) Kufungua Mlango wa Adui kukuhubiri nani zaidi kati ya mafataki na ndoa.
Kuvutwa kumbukumbu ya ‘sex’ ya kabla ya Ndoa kupambanishwa na ndani ya Ndoa.  Ni rahisi sana kugundua nani zaidi kwa vile Tendo ni lile lile ila tofauti ni kabla ya Ndoa ni HARAMU na Ndani ya Ndoa ni HALALI. Sasa ukizoea dhambi hii Kanisani tena kwa siri, hakuna toba ya kweli, haujatengwa iabishwe, haijulikani kwetu ila mwili wako unajua ni HATARI.

Unaweza kuoa/kuolewa na mume mzuri/mke mzuri tu lakini tatizo likawa hakidhi uhitaji wa kimapenzi kwa namna ya mwili wako ulivyouzoesha kabla ya kuoa/kuolewa hili tayari ni tatizo kubwa linalotikisa NDOA.

Tunapomalizia madhara hayo ishirini [20] kati ya mengi ya kufanya mapenzi kabla ya Ndoa; tunakusihi wewe ambaye hujaguswa na hujagusaUsijaribu na mwenye Ukuta wa Roho MtakatifuUsitende dhambi tena. Wote tuipate THAWABU ya wanaovumilia hadi mwisho-Mathayo 24:13.

4.     HITIMISHO
i)      Ishi ukijua kuwa umekufa kwa dhambi unaishi kwa roho-Warumi 8:5-10;
Na ukiishi kwa roho hautazitimiza kamwe tamaa za mwili/ujanani-Gala 5:16.

ii)   Ishi kwa tahadhari sana huku ukijiangalia usianguke – 1Kor 10:12-13.

iii) Usijiamini kupita kiasi [over confidence] kwa kigezo cha andiko Rumi 6:2-11.
Kuna watu wamejiamini kupita kiasi kwa andiko hili, busu maiti mara inafufuka.

iv)  Ishi kama mtumwa wa Mungu uko huru lakini huko huru- 1Pet 2:16; Rum 6:12-14.
Kijana wewe ni mtumwa wa Mungu na Yesu ni Bwana wako mipaka ni lazima.
Mipaka katika Mavazi, Marafiki, Mazungumzo, matendo, mahusiano, masaidiano, muda, mikutano [mahali pa kuwepo], mawasiliano kwa ujumla, Mipaka kwa mwenendo mzima hasa kwa jinsia 2 hizi tofauti-ni hatari kugandana kama ruba, ni hatari kufatana kama kumbikumbi, ni hatari kuambatana gizani sisi ni wa nuruni. Mungu akupe neema ya kushinda mwili unaokuvuta huko na uweke mipaka kila eneo kwa damu ya Yesu na kuhakikisha huvuki wigo huo ili UTUNZE UJANA WAKO na Utumishi wako usilaumiwe kwa kusababisha mwenyewe tuhuma hizo.  Vyanzo vya Vijana wengi kulaumiwa hata kama hatujafanya jambo ni KUKOSA MIPAKA.  Kuutumia vibaya uhuru wetu na undugu wetu katika Kristo ila wewe usiwe hao.

v)    Ishi kwa kufuata hekima ya Mungu si wanadamu – Yakobo 3:17; Rumi 16:19b.

vi)  Subiri wakati wa Bwana [Ndoa] – Mith 6:20; 26; 7:1-5; 21:27; Mhubiri 3:1. Usijidhalilishe kwa mtu asiye wako, mara Mfalme ‘anamatege’ au ‘anamaganda’ yatanadiwa mji mzima. Malkia ‘anamakovu’ anayaona fataki. Mtu aliyewako hata akute mapungufu atakupokea jinsi ulivyo maana amepewa na Bwana. Subiri Ndoa.

vii)  Jizoeshe kuliishi Neno la Mungu ili uwe na adabu neno huadibisha- 2Tim 3:16.
Biblia inasema wazi neno hutuadibisha, hututia adabu ya kuongea, kutenda n.k.

viii)  Inawezekana kabisa kutunza ujana wako hadi ndoa–Marko 10:27; Matha 19:26.
Yasioyowezekana kwa wanadamu kwa Mungu yote yanawezekana, AMEN.

**MWISHO**


Share To:
Magpress

Calvin Petro

Kwa Moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na Maagizo yako. Moyoni mwangu nimeliweka Neno lako Nisije nikakutenda dhambi. (Zaburi 119:10-11).

Post A Comment:

3 comments so far,Add yours

  1. Ninashukuru sana kwa ujumbe huu mzuri sana. Mungu aibariki kazi ya mikono yako.

    JibuFuta
  2. ...somo zuri sana
    Mungu atusaidie tuweze kuyafanyia kazi.

    JibuFuta