Haikuanzishwa na wanadamu bali mungu ndiye aliyeanzisha taasisi hii… imeanzishwa na mungu ambaye ni roho, uwe na uhakika haiwezi kuendeshwa kwa kutegemea akili, hekima na maarifa ya wanasaikolojia, washauri wa mahusino nakadhalika.
Kama ni ndoa lazima kwanza msingi wake uwe imara; na msingi sahihi wa ndoa imara na ya kudumu lazima uwe mungu ambaye ni roho; lazima msingi wa ndoa ya uhakika uwe neno la mungu!
Ndoa si taasisi ya hisia, hisia zinakuja baadaye cha kwanza ni kuwa na msingi sahihi wa mungu na neno lake kuhusu ndoa na mahusiano kwa ujumla!
Hawa washauri wa mahusiano ni waburudishaji tu; hawawezi kukupa kanuni za kweli za kukufanya uwe na ndoa ya ushindi, bali wataishia kukutia moyo, wao ni sawa na pampu inayopuliza hewa kwenye puto lenye tundu.

Hawawezi kuona tundu bali juhudi zao zitagonga mwamba baada ya muda mfupi sana.

Kama ndoa ni wazo la mungu, na si wazo la adamu, uwe na uhakika adamu anahitaji wazo la mungu kukaa na kumfurahia hawa wake aliyeletewa na mungu… adamu akimtafuta hawa kwa mbinu na kanuni zake anazojua, hawezi kuthibitika…ni rahisi namna hiyo!
Share To:
Magpress

Calvin Petro

Kwa Moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na Maagizo yako. Moyoni mwangu nimeliweka Neno lako Nisije nikakutenda dhambi. (Zaburi 119:10-11).

Post A Comment:

0 comments so far,add yours