Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho. —YEREMIA 29:11

Iwapo una picha mbaya binafsi kujihusu, tayari imeathiri vibaya mambo yake ya kale, lakini unaweza kuponywa na kutoruhusu ya kale kujirudia. Ninakuhimiza kusahau yaliyopita hata mambo yoyote hasi ambayo umehisi kujihusu na kujisukuma mbele kuelekea vitu ambavyo Mungu amekuwekea.

Mungu ana mpango mwema na kusudi kwa kila mmoja wetu na njia maalum na wakati mtimilifu wa kuyafanya yatimie, lakini sio sisi wote tunayaona haya. Wakati mwingi tunaishi chini ya kiwango cha maisha ambayo Mungu anakusudia tufurahie.

Kwa miaka mingi sikutumia haki na faida zangu kama mwana wa Mungu. Ingawa nilikuwa Mkristo na kuamini nitaenda mbinguni nitakapofariki, sikujua kwamba kuna jambo ambalo lingefanywa kuhusu maisha yangu yaliyopita, yaliyopo na yajayo. Nilikuwa na picha mbaya kujihusu, na ikaathiri maisha yangu ya kila siku, pamoja na mwono wangu wa siku zijazo.

Leo unaweza kukubali upendo wa Mungu juu yako na uufanye upendo wake msingi wa kujipenda na kujikubali. Pokea hakikisho lake, ukijua kwamba unabadilika na kuwa vile anavyotamani uwe. Halafu uanze kujifurahisha—ulipo—ukiwa njiani kuelekea ukomavu mkamilifu wa kiroho.

Acha Mungu awe Mungu katika maisha yako. Mweke katika kiti cha dereva. Anajua analofanya.

 

Share To:
Magpress

Calvin Petro

Kwa Moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na Maagizo yako. Moyoni mwangu nimeliweka Neno lako Nisije nikakutenda dhambi. (Zaburi 119:10-11).

Post A Comment:

1 comments so far,Add yours

  1. Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na akaondoka kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki yangu aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu ili kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.

    Mwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwa ajili yangu - na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.

    Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.

    Lakini sio hivyo tu - Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyozunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.

    Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote - huzuni, bahati mbaya, au kuchanganyikiwa - usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.

    Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159
    dawnacuna314@gmail.com

    JibuFuta