Mambo ya nyuma yasikufanye ushindwe kuifurahia leo yako au kupanga mipango kwa ajili ya kesho yako. Hakuna ambaye hajawahi kuumizwa iwe ni maisha/ mtu / watu au hali. Kinachotofautisha ni uamuzi wa kuachilia maumivu na machungu ya nyuma na kusonga mbele. Kuendelea kuyashikilia na kuyabeba kama bango haiondoi uhalisia kuwa yametokea wala hakufanyi leo yako kuwa nzuri.

Tambua kuwa maisha yako ni jukumu lako na si mwingine yeyote. Haijalishi umeumizwa vipi, unawajibika kuishi maisha yako kwa furaha na kufanya bidii ili kesho iwe bora zaidi. Aliyekukosea au kukusababishia maumivu hawajibiki kukupa furaha wala kukuondolea maumivu, ni jukumu lako asilimia mia. Amka sasa, jikung’ute maumivu yote na uchungu wa yaliyopita na usonge mbele.

Si kwa uweza wala nguvu zetu bali kwa msaada wa Mungu.



chanzo: https://womenofchrist.wordpress.com

Share To:
Magpress

Calvin Petro

Kwa Moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na Maagizo yako. Moyoni mwangu nimeliweka Neno lako Nisije nikakutenda dhambi. (Zaburi 119:10-11).

Post A Comment:

0 comments so far,add yours