Mwaka 1997 tulipokea barua na simu nyingi toka kwa watu wa Mungu mbalimbali wakihitaji maombi kwa ajili ya matatizo yaliyokuwa yanawasumbua katika maeneo ya kifedha. Wengine biashara na kazi zao vilikuwa haviendi vizuri - nakadhalika.
Tulikaa na jambo hili katika maombi. Tarehe 24 Septemba 1997 saa kumi na nusu asubuhi tukiwa katika maombi Bwana Yesu alisema nasi katika mioyo yetu ujumbe ufuatao ambao tunaamini utakusaidia hata wewe. Bwana Yesu alituambia hivi:


roho ya mpinga Kristo ndiyo iliyoshambulia mafanikio ya kifedha katika watu wangu,

Imeelekeza mashambulizi katika mafanikio ya roho zao (na nafsi zao) maana nimesema mtafanikiwa katika mambo yote kwa kadri roho zenu zifanikiwavyo,

Kufanikikiwa kwa roho zenu kunategemea kufanikiwa kwa nafsi zenu. Mtafanikiwa katika roho zenu kwa kadri nafsi zenu zifanikiwavyo, na matokeo yataonekana katika mambo yote

Nafsi zenu zifanikiwavyo zinategemea utendaji wenu wa Neno langu. Ikiwa utendaji wenu wa Neno ukiwa hafifu, na kufanikiwa kwa nafsi zenu kunakuwa hafifu. Kufanikiwa kwa nafsi zenu kukuwa hafifu na kufanikiwa kwa roho zenu kunakuwa hafifu, kwa hiyo kufanikiwa katika mambo yote kunakuwa hafifu pia.

Ndiyo maana nasema roho ya mpinga Kristo imeelekeza mashambulizi yake katika kupinga, kuzuia, na kuchelewesha mafanikio yenu katika roho na nafsi zenu.

Lakini mnaweza kushinda kwa kusimama katika Neno langu ambalo ni upanga wa Roho mikononi mwenu.

Nimesema katika Yoshua 1:8 ya kuwa mtafanikiwa ikiwa mambo matatu yatafanyika juu ya Neno langu:
(a) Lisiondoke kinywani mwenu
(b) Mlitafakari wakati wote
(c) Na kudumu kulitenda

Sasa angalia mmesimamaje katika maeneo hayo matatu. Maana hizo ni mbinu za kulitumia Neno langu kama silaha ya kumshinda adui

Mkisimama katika Neno langu ninavyotaka mtavuna mafanikio sana kwa wakati wangu msipozimia na kukata tamaa katika mioyo yenu.

roho ya mpinga Kristo inawakatisha tamaa kwa kuwaangaliza matokeo ya upungufu mlionao badala ya kuangalia ahadi zangu na matokeo yake.

Kwa kadri mnavyoangalia matokeo ya upungufu mlionao, ndivyo mnavyozidi kutafakari juu ya upungufu mlionao. Kwa kadri mnavyozidi kutafakari juu ya upungufu mlionao, ndivyo mnavyozidi kukiri na kushuhudia upungufu mlionao na matokeo yake.

Kumbuka mnayafunga mafanikio yenu kwa maneno ya vinywa vyenu yanayotoka katika nafsi zisizotafakari ahadi zangu na matokeo yake.

Mimi si mtu hata niseme uongo. Nililolisema katika Neno langu nimesema nitalitimiliza. Napenda kufanikiwa kwenu kuliko nyinyi mnavyopenda kufanikiwa kwa watoto wenu. Msikubali adui ayumbishe macho yenu na mioyo yenu isione uaminifu wangu.

Mkisimama katika neno langu na kupigana hivyo vita vizuri vya imani mlivyo navyo;
- mtashangilia ushindi wakati kuta hazijaanguka bado,
- mtatangaza ushindi wakati bado upinzani wa adui umesimama,
- mtaona mafanikio wakati bado mmezungukwa na upungufu,

Kumbuka neno langu linatangaza ushindi katika roho kwanza kabla ya haujaonekana kwa nje. Ndicho kilimchomsaidia Ibrahimu wakati anasubiri mtoto wake. Na ndicho kilichonisaidia na mimi pale masalabani - nilishangilia ushindi dhidi ya adui hata kabla sijafufuka. Daudi naye aliuona ushindi wakati bado Goliati amesimama mbele yake.

Kila mtu atakuja kwangu na kuuliza nimpe Neno la kusimamia katika vita alivyo nayo. Hamuwezi kushinda pasipo Neno.

Haya ndiyo machache tuliyoyapokea kutoka kwa Bwana Yesu tulipofanya maombi ya kuuliza kwa nini watu wengi wa Mungu wamekuwa hawafanikiwi vizuri katika eneo la fedha. Ingawa Bwana alisema nasi mwaka 1997 tunaamini bado ujumbe una nguvu ndani yake ya kukusaidia. Tafakari maneno ya ujumbe huu, weka katika matendo yaliyomo - na Mungu atakusaidia!

Ahsante,

Mwl. Christopher Mwakasege

 

Share To:
Next
This is the most recent post.
Previous
Taarifa za zamani
Magpress

Calvin Petro

Kwa Moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na Maagizo yako. Moyoni mwangu nimeliweka Neno lako Nisije nikakutenda dhambi. (Zaburi 119:10-11).

Post A Comment:

2 comments so far,Add yours

  1. Ushuhuda Wangu wa Dhati 💖

    Baada ya baba yangu mdogo kuniacha kwa miezi saba ndefu, nilivunjika kabisa. Alinifungia kwenye mitandao yote ya kijamii, akasafiri mbali, na hakukuwa na njia ya kumfikia. Nilikaribia kukata tamaa juu yetu, lakini ndani kabisa nilijua singeweza kupata mtu yeyote ambaye angenipenda na kunitendea jinsi alivyonitenda.

    Siku moja, bosi wangu kazini aliona jinsi nilivyokuwa na huzuni na akanitambulisha kwa Dk. Dk. Dawn alisikiliza hadithi yangu na akaahidi kwamba mpenzi wangu atanirudia ndani ya siku tatu. Kusema kweli, sikuamini mwanzoni—lakini kwa mshangao mkubwa zaidi, siku ya tatu simu yangu iliita. Ilikuwa ni yeye! Alikuwa akilia na kuomba msamaha, akisema hataniacha tena.

    Tangu siku hiyo, uhusiano wetu umekuwa wenye nguvu na mzuri zaidi kuliko hapo awali. Amekuwa akinipenda na kunijali sana mimi na mtoto wetu, na sasa tunafunga ndoa baada ya miezi miwili tu! ❤️

    Shukrani zote kwa Dk. Dawn, ambaye kwa kweli aliwezesha jambo lisilowezekana. Ninampendekeza kwa moyo wote kwa yeyote anayekabiliwa na changamoto katika:

    Masuala ya mahusiano au ndoa

    Ugonjwa au magonjwa

    Ugumba au matatizo ya bahati nasibu

    Kesi za mahakama au kurejesha mali


    Dk. Dawn kweli hutatua matatizo kwa ufanisi na hurejesha furaha katika maisha ya watu.

    Wasiliana na Dr. Dawn kwenye WhatsApp: +2349046229159
    Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com

    JibuFuta
  2. 🌹 Ushuhuda Wangu Kuhusu Dkt. Dawn – Mtu Aliyerejesha Nyumba Yangu na Furaha Yangu

    Nataka kushiriki ushuhuda wangu wa dhati kuhusu jinsi Dkt. Dawn alivyobadilisha maisha yangu kabisa.

    Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na alikuwa ameenda kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.

    Mwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwangu — na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.

    Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.

    Lakini si hayo tu — Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyokuwa ikizunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.

    Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote — huzuni, bahati mbaya, au mkanganyiko — usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.

    Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159
    Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com

    JibuFuta