Kumbuka upendo wako wa kwanza kwa mkeo. Kumbuka yule binti uliyekuwa unakosa usingizi kwa ajili yake, ulivyokuwa unapita pita karibu na kwao ili walau umuone moyo wako utulie. Uliyekuwa huwezi kulala kabla hujaisikia sauti yake. Kumbuka jinsi moyo ulivyokuwa unadunda siku ya kwanza kumueleza ya moyoni na jinsi gani ulivyojaa furaha alipokubali kuwa nawe siku zote za maisha yako.
 
Je kwanini leo hii unamuona hafai tena? Leo hii msichana aliyekuwa mpenzi wa moyo wako unamtendea visivyo tena bila hata kujali? Je ule upendo wa kwanza umeenda wapi? Amka katika usingizi wako, huyo mkeo ndiye yule yule binti uliyekuwa huambiwi wala husikii juu yake, uliyeapa kumlinda, kumfurahisha na kuwa naye siku zote za maisha yako.

Chukua dakika chache ufikirie mwanzo wa penzi lenu, na pia andika kabisa vitu ambavyo ulikuwa unamfanyia na uso wake unachanua kwa furaha. Sasa azimia kuyafanya hayo yote kuanzia sasa. Hata kama kuna uzito ndani yako, jisukume kutenda na hakika hutajuta. Usiangalie amefanya nini na amekosa nini bali angalia ule upendo wako wa kwanza na dhamiria kuurudisha upya katika ndoa yako.

Nakwambia ukifanya hivi utakuja kunishuhudia jinsi furaha ya ndoa ilivyoongezeka mara dufu.


1PETRO 4:8,   1WAKORINTHO 13:1-13


Share To:
Magpress

Calvin Petro

Kwa Moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na Maagizo yako. Moyoni mwangu nimeliweka Neno lako Nisije nikakutenda dhambi. (Zaburi 119:10-11).

Post A Comment:

1 comments so far,Add yours

  1. Asante sana kwa maelezo muhimu kuhusu kumpata mwenzi wa maisha

    JibuFuta